
Sunday
Ludacris Design kakopi Swagger za B12 katika Serengeti Fiesta 2011

Friday
Ludacris akasign kitabu cha wageni kutoka Hollywood niliokutana nao

Thursday
Tuesday
Nick Minaj Awa Balozi wa MAC Cosmetics

Kampeni ambayo itazinduliwa mwezi wa pili mwaka ujao, ambapo Nick atakuwa ndo msemaji wao na sura ya kampuni hiyo, Wakati huo huo Nick Minaj anatoa lipstick yake mwenyewe ambayo itakuwa ina rangi ya pink, nahisihii ni kutokana na dada huyu kuwa mpenzi wa rangi ya pink.
Kwa hivi sasa Nick minaj Yupo Miami akipiga picha za matangazo kwa ajili ya kampeni hii. kupitia ukurasa wake wa twitter Nick Minaj ameandika "hii shoot ni GAG, yaani siwezi kusubiri kuona jinsi watu wavyopendeza na hii Lipstick yangu mpya,kaeni tayari"
Monday
Tanga Yasimama Wima na Burudani ya Serengeti Fiesta



Thursday
Muonekano wako Uwapo Ufukweni

Ufukweni au beach kama wengi mlivyozoea mara nyingi ni eneo ambalo huwa tunaenda kupunga upepo na kutuliza akili zetu kutokana na yale tuliyopitia kwa kipindi kilichopita! familia nyingi au vijana wengi kama nijuavyo mimi hupenda kwenda ufukweni wakati wa weekend hii ni kutokana na kuwa ndio wakati pekee tunapata nasi.
Tukumbushane mambo ya muhimu uendapo ufukweni ili usiwe tofauti na wenzio utakaokutana nao huko, kwa vijana wakiume hizi ndizo kaptula zinazotufaa kwakuwa hazibaki na maji mwili wala kushika maungo yetu maana kuna watu huwa hawana amani kuogelea na nguo zao za ndani kwakuwa huwa wanahisi wanajichora maungo yao, hivyo basi ukipata kaptula kama hizi mambo yako yatakuwa salama kabisa.








Kabla ya kutumia lotion hizi jitahidi kumuona mtaalamu wa ngozi ili uweze kupata lotion inayoendana na ngozi yako maana lotion nyingi za jua zimetengenezwa kwa ngozi za watu weupe (wazungu)
Wednesday
R Kelly akimbizwa Hospital


Monday
DARASA: Epuka Msongo wa Mawazo (Stress)



1.Tambua chanzo cha msongo wa mawazo ulionao, je ni kazi yako na eneo lako la kazi?? je ni maisha yako binafsi (Lifestyle), rafiki au ndugu zako au wapenzi wa kazi zako??
2. Tambua huwa unakuwa katika hali gani pindi unapokuwa na msongo wa mawazo.
Jinsi ya kuepukana na Stress
Kuna baadhi ya Stress ambazo zinaepukika na nyingine ni ngumu kuziepuka ila unapaswa kujua jinsi ya kutatua shinikizo la msongo wa mawazo
1. Jifunze kusema "hapana" hii ni katika mambo yako binafsi au kazi yako, unaitumiaje hii hapana? unajua maofisini kuna swala la kupeana vikazi visivyoeleweka hata vimetokea wapi, yaani hujamaliza hili unaletea jingine hata kama sio kazi yako... sasa jifunze kukataa hizi kazi zisizo za kwako ili mradi tu mfurahishe tu. hivyo hivyo vitu vidogo vidogo ndivyo vinavyokuletea msongo wa mawazo.
2.Jiepushe na watu ambao mara nyingi wanakusababishia Stress, unajua ukikaa chini na kufikiria utagundua kuna mtu flani au kundi flani la watu ndo linalokuleta msongo wa mawazo, sasa kaa nao mbali kabisa.
3. Simamia mazingira yanayokuzunguka
mazingira yanakuzunguka yanaweza kuwa sababu ya stress zinazokukumba, mazingira yapo nayozungumzia mimi hapa? njia unayotumia kwenda kazini au kurudi nyumbani ina foleni sana? hiyo nayo inawea kuwa sababu ya stress ulizonazo, lakufanya epuka matumizi ya barabara kwa wakati huo, mazingira ya soko wakati wakufanya manunuzi ya bidhaa mbali mbali yanakupa stress? nenda katika supermarket maana kwa kiasi flani kuna utulivu na hali ya hewa nzuri
4.Epuka Hasira za haraka, kuna ya mambo yanayohusu dini,siasa au maisha yako binafsi huwa yanakupa msongo wa mawazo basi jitahidi kuepukana nayo katika mazungumzo yako ya kila siku kwasababu yatakupa hasira na kukufanya ukasirike na hili hupelekea kuwa na msongo wa mawazo, ukiingia sehemu ukakuta watu wanaongelea swala hilo epuka nao ili usiweze kuchangia na kujikuta unaingia katika mgogoro wa nafsi
5.Tengeneza orodha ya vitu anavyotaka kufanya sikuhiyo asubuhi tu ukiamka, mara nyingi unapaswa kujua mambo ambayo ni ya lazima kuyafanya kwa siku ambayo unaianza ili ikifika jioni usiwe na viporo, katika orodha yako tenganisha orodha hiyo kwa vitu vya lazima kufanya na vitu vya kawaida ambavyo hata usipovifanya hazitakuharibia ratiba yako. kujua kipi cha lazima ni moja ya njia kubwa ya kupunguza msongo wa mawazo.
Naomba niishiw hapa kwa leo maana nimewaonjesha yale ninayoyajua na ambayo nimejifunza, swala la kuondoa msongo wa mawazi linapaswa kuangaliwa kiundani zaidi maana ni pana sana, hapa juu nimeongelea kuepuka stress ambazo si za muhimu ila kuna swala la saikolojia ambalo sijaligusa kwakuwa mimi si mtaalam wa saikolojia. siku nikijua mengi zaidi kuhusu stress nitatoa darasa zaidi.
Subscribe to:
Posts (Atom)