FOR WEDDING PLANNING, FASHION DESIGNING, ART DIRECTION AND STYLING CALL +255 717 514179

Sunday

Ludacris Design kakopi Swagger za B12 katika Serengeti Fiesta 2011

Hamis Mandi aka B12 ndivyo anavyojulikana na wengi wa wasikilizaji wa kipindi anachokiendesha ndani ya cloudsfm (XXL) yeye ndo alikuwa mtu wa kwanza kumuona alipokuja backstage ya Fiesta kwa ajili ya kushirikiana na watangazaji wengine kuendesha Shughuli nzima ya Fiesta kwa mwaka huu, alikuwa chini kavaa Sneaker Nyeusi na ana pensi ya Army pamoja na tishirt nyeusi, haikuchukua muda mrefu kama katika time za tano hivi mwanamziki kutoka marekani Ludacris nae akaingia backstage akiwa na kiundi lake, ila nilipomwangalia kwa makini nikaona kavaa sawa sawa na B12, angalia hizi picha then nipe tathimini yako kama mimi nimekosea

Friday

Ludacris akasign kitabu cha wageni kutoka Hollywood niliokutana nao

Always huwa nafurahi pindi napokutana na watu waliweza kuendesha maisha yao na kuajiri wengine kupitia kazi zao! nilijisikia faraja sana nilipokutana na Naomi Campbell mmoja wa mastaa wa kubwa katika fashion duniani, kutoka hapo nikawa na kiu ya kumeet more celebrities from all over the World, haikuchukua muda Mrefu nikakutana na Star wa filamu Africa Ramsey Noah, Shaggy akafuata na Sasa nimekutana na Ludacris, kila nafasi kama hizi zinapotokea huwa napenda kuzitumia vizuri si mbaya my portfolio ikiwa na picha nilizopiga na Celebrities walifanikiwa kimaisha, Mungu sikiliza maombi yangu niweze kufanikiwa na kuja kuwa role model kwa wale wanaonipenda na kunisupport kwa kile kidogo ninachokifanya hivi sana.

Thursday

My weekend in Arusha

Ona picha kwanza maelezo yatafuta nikiwa nimetulia.


















Tuesday

Nick Minaj Awa Balozi wa MAC Cosmetics

Mwimbaji wa Rap Nick Minaj Inawezekana akawa anafata nyayo za Lady Gaga, Baada ya Hivi karibuni amesaini mkataba na Kampuni kubwa duniani ya Vipodozi ya MAC, Nick atakuwa balozi ya kampeni mpya ya bidhaa hizi inayojulikana kama VIVA GLAM 2012,

Kampeni ambayo itazinduliwa mwezi wa pili mwaka ujao, ambapo Nick atakuwa ndo msemaji wao na sura ya kampuni hiyo, Wakati huo huo Nick Minaj anatoa lipstick yake mwenyewe ambayo itakuwa ina rangi ya pink, nahisihii ni kutokana na dada huyu kuwa mpenzi wa rangi ya pink.

Kwa hivi sasa Nick minaj Yupo Miami akipiga picha za matangazo kwa ajili ya kampeni hii. kupitia ukurasa wake wa twitter Nick Minaj ameandika "hii shoot ni GAG, yaani siwezi kusubiri kuona jinsi watu wavyopendeza na hii Lipstick yangu mpya,kaeni tayari"

Monday

Tanga Yasimama Wima na Burudani ya Serengeti Fiesta

This weekend nilikuwa Tanga katika Fiesta, naonekana kwa mbali katika picha hiyo hapo juu nikiwa na Antu na Pako mmoja wa madancer mahiri Bongo,Kwakweli i had a very good time katika mji huu maana ndio ilikuwa mara ya kwanza kutia kambi Tanga, kuna mengi niliyofaidi ila kwa upande wa burudani on stage, hawa ndio walionipagawisha!!
Shetta ni mmoja wa wasanii ambao kwangu nilikuwa nawaona ni wakawaida sana ila daah show aliyoifanya Tanga napenda kusema yeye ni mmoja wa wasanii wazuri juu ya jukwaa, napenda show ya kucheza aliyofungua nayo kabla hajaanza kuimba!! Shetta Your the Best.

Mwana FA utabaki kuwa kaka yao katika muziki, one man on stage na bado unaenjoy with no complains?? alifunika mbaya na ile ngoma ya Unanijua au unanisikia??

Linex wa Mama Halima he was the BEst kwa upande wangu, watu walikuwa wamepoooa lakini aliwaamsha kwa shangwe za ajabu nahisi ni kutokana na muziki wake kupendwa sana ndani ya Tanga.

Katika watu ambao hawajali wewe utasema nini as long he is doing what he loves the most ni Bob Junior, alipiga show ya nguvu na upande wa mavazi alinikosha sana, Respect kwako Bob Junior

For me, He is a king of soul, muziki wake unagusa hisia za ndani kabisa kwa yule mpenda burudani ya muziki, Ben Paul alinirusha vya kutosha na new track yake inayojulikana kama Number one fan.

After all those shows nje ya Tanzania unategemea nini Tena kutoka kwake?? mwite mkali wa Stage Ally Kiba mzee wa Dushele, tulidusheleka kweli kweli tanga.

Thursday

Be inspired with His trends- Trey Songz

Kitu cha original Gucci Belt kiunoniI like Striped vest inside his shirtCotton shirts kwa ufukweni iko poa piaKiatu chini hapo

Muonekano wako Uwapo Ufukweni



Ufukweni au beach kama wengi mlivyozoea mara nyingi ni eneo ambalo huwa tunaenda kupunga upepo na kutuliza akili zetu kutokana na yale tuliyopitia kwa kipindi kilichopita! familia nyingi au vijana wengi kama nijuavyo mimi hupenda kwenda ufukweni wakati wa weekend hii ni kutokana na kuwa ndio wakati pekee tunapata nasi.Tukumbushane mambo ya muhimu uendapo ufukweni ili usiwe tofauti na wenzio utakaokutana nao huko, kwa vijana wakiume hizi ndizo kaptula zinazotufaa kwakuwa hazibaki na maji mwili wala kushika maungo yetu maana kuna watu huwa hawana amani kuogelea na nguo zao za ndani kwakuwa huwa wanahisi wanajichora maungo yao, hivyo basi ukipata kaptula kama hizi mambo yako yatakuwa salama kabisa.

Kitu cha muhimu kuzingatia wakati wa kununua kaptula ya kuogelea, chagua rangi zinazoendana na rangi yako ya ngozi, mtu mweusi hauendani na rangi kali, kama orange, njano mkozo au kijani kikali... tafuta kaptula za rangi iliyopoa.Ndugu zangu kutokana na mchanga wa Beach hatuendi na Raba ila sandals au kwakiswahili fasaha viatu vya wazi, jitahidi kupata sandals nyepesi zisizo nzito ili uweze kutembea kwa wepesi katika ule mchanga wa baharini

Zingatia rangi ya Sandals inayoendana na kaptula utayaokuwa umevaa ili ung'ae na kuvutia, who knows? inaweza kuwa your luck day kama uko single ukamvutia binti ambaye anaweza kuwa yupo ufukweni kwa siku hiyo

mara nyingi kuna vumbi jepesi ambalo huwa linatimka kutokana na upepo wa baharini, jitahidi kuwa na sun glasses kwa ajili ya kuzuia vumbi hilo kuja moja kwa moja machoni kwako, huwa kunakuwa na jua kali wakati mwingine hivyo miwani hiyo hiyo itakusaidia kuepukana na miale mikali ya jua.Miwani ipo ya rangi tofauti, chagua inayokufaa

Mwisho kabisa unahitaji lotion za jua kwa ajili ya ngozi yako, jua huwa linakuwa kali sana na linaweza kuharibu ngozi yako usipokuwa makini, hivyo ningependa kukushauri kuwa na sun lotion ambayo inaendana na ngozi yako.


Kabla ya kutumia lotion hizi jitahidi kumuona mtaalamu wa ngozi ili uweze kupata lotion inayoendana na ngozi yako maana lotion nyingi za jua zimetengenezwa kwa ngozi za watu weupe (wazungu)

Wednesday

R Kelly akimbizwa Hospital

Mwanamziki R.kelly jana jioni alikimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu ya haraka! Habari kutoka kwa wasemaji wa mwanamziki huyu amesema kuwa sababu kubwa ya Rkelly kukimbizwa jana hospital ni kutokana na maumivu makali aliyokuwa anayapataka katika koo lake.
Habari zaidi zinasema kuwa sababu kubwa ya maumivu hayo yanaweza kuwa yamesababishwa na kukauka kwa koo, hivyo ataendela kuwepo hapo hospitali mpaka hali yake itakapokuwa imekaa sawa!

Chicago NorthWestern Memorial Hospital ndipo R.Kelly anapopata matibabu

Monday

One of best songs for now,Beyonce - End Of Time (Live )

DARASA: Epuka Msongo wa Mawazo (Stress)

Mara nyingi tumekuwa tukikumbwa na msongo wa mawazo kutokana na shughuli zetu za kila siku katika maisha, Endapo wewe ni mdau wa burudani kwa upande wowote, labda ni mwanamziki, mtangazaji, muigizaji,mwanamitindo au hata mshereheshaji katika hizi kazi zetu tunakutana na watu wengi kila siku na wanakuwa na hamu ya kukujua kutokana na kazi unayoifanya au nia mbali mbali wanazozijua wao wenyewe, Sasa kitendo cha kuwa na watu wengi karibu inamaanisha na mahitaji kutoka kwako yanaongezeke, trust me kama unafamilia ambayo inakuangalia, wasanii wenzako wanakuangalia na wapenzi wa kazi yako nao wanakuangalia Lazima utakumbana na msongo wa mawazo, maana utakumbwa na bili za kuzilipia, watu wa kuwasaidia kiushauri na hata kimahitaji au kushiriki shughuli mbalimbali ukiachilia mbali kazi yako binafsi.. Je ni jinsi gani unaweza kuepuka msongo wa mawazo kutokana na hayo yote?




1.Tambua chanzo cha msongo wa mawazo ulionao, je ni kazi yako na eneo lako la kazi?? je ni maisha yako binafsi (Lifestyle), rafiki au ndugu zako au wapenzi wa kazi zako??

2. Tambua huwa unakuwa katika hali gani pindi unapokuwa na msongo wa mawazo.

3. Mara nyingi kitu gani huwa kinakusaidia kupunguza huo msongo wa mawazo awali


Jinsi ya kuepukana na Stress

Kuna baadhi ya Stress ambazo zinaepukika na nyingine ni ngumu kuziepuka ila unapaswa kujua jinsi ya kutatua shinikizo la msongo wa mawazo


1. Jifunze kusema "hapana" hii ni katika mambo yako binafsi au kazi yako, unaitumiaje hii hapana? unajua maofisini kuna swala la kupeana vikazi visivyoeleweka hata vimetokea wapi, yaani hujamaliza hili unaletea jingine hata kama sio kazi yako... sasa jifunze kukataa hizi kazi zisizo za kwako ili mradi tu mfurahishe tu. hivyo hivyo vitu vidogo vidogo ndivyo vinavyokuletea msongo wa mawazo.


2.Jiepushe na watu ambao mara nyingi wanakusababishia Stress, unajua ukikaa chini na kufikiria utagundua kuna mtu flani au kundi flani la watu ndo linalokuleta msongo wa mawazo, sasa kaa nao mbali kabisa.


3. Simamia mazingira yanayokuzunguka

mazingira yanakuzunguka yanaweza kuwa sababu ya stress zinazokukumba, mazingira yapo nayozungumzia mimi hapa? njia unayotumia kwenda kazini au kurudi nyumbani ina foleni sana? hiyo nayo inawea kuwa sababu ya stress ulizonazo, lakufanya epuka matumizi ya barabara kwa wakati huo, mazingira ya soko wakati wakufanya manunuzi ya bidhaa mbali mbali yanakupa stress? nenda katika supermarket maana kwa kiasi flani kuna utulivu na hali ya hewa nzuri


4.Epuka Hasira za haraka, kuna ya mambo yanayohusu dini,siasa au maisha yako binafsi huwa yanakupa msongo wa mawazo basi jitahidi kuepukana nayo katika mazungumzo yako ya kila siku kwasababu yatakupa hasira na kukufanya ukasirike na hili hupelekea kuwa na msongo wa mawazo, ukiingia sehemu ukakuta watu wanaongelea swala hilo epuka nao ili usiweze kuchangia na kujikuta unaingia katika mgogoro wa nafsi


5.Tengeneza orodha ya vitu anavyotaka kufanya sikuhiyo asubuhi tu ukiamka, mara nyingi unapaswa kujua mambo ambayo ni ya lazima kuyafanya kwa siku ambayo unaianza ili ikifika jioni usiwe na viporo, katika orodha yako tenganisha orodha hiyo kwa vitu vya lazima kufanya na vitu vya kawaida ambavyo hata usipovifanya hazitakuharibia ratiba yako. kujua kipi cha lazima ni moja ya njia kubwa ya kupunguza msongo wa mawazo.


Naomba niishiw hapa kwa leo maana nimewaonjesha yale ninayoyajua na ambayo nimejifunza, swala la kuondoa msongo wa mawazi linapaswa kuangaliwa kiundani zaidi maana ni pana sana, hapa juu nimeongelea kuepuka stress ambazo si za muhimu ila kuna swala la saikolojia ambalo sijaligusa kwakuwa mimi si mtaalam wa saikolojia. siku nikijua mengi zaidi kuhusu stress nitatoa darasa zaidi.